Saturday, April 7, 2012

kifo cha kanumba na ujauzito wa LULU

LULU UJAUZITO WA KANUMBA BADO UNAO AU UMEUTOA? NATAMANI UJIBU YES

Mdogo wake Kanumba ktk Interview na medias leo asubuhi nyumbani kwa The Late Steven Kanumba

Si inafahamika kuwa Actress Lulu anashikiliwa na polisi ili ahojiwe kuhusu mazingira ya Kifo cha Kanumba,
Sasa Kama ningekua mmoja kati ya maofisa wa upelelezi wa kifo cha The Late Steven Kanumba, leo hii mara baada ya Mwanasheria wa Lulu Kufika basi swali langu la kwanza ningemuuliza Je Ule ujauzito uliopewa na Kanumba uliutoa ama? Natamani ujibu Yes, ili wengi wetu tufarijike, wala usishtuke na hilo swali,

Eeh maana mwezi uliopita zilisambaa taarifa kuwa wawili hao wana mahusiano ya kimahaba, lakini wakakana, na kuhusu Lulu kuwa na ujauzito na Kanumba pia aliruka futi sita,
Sasa Leo hii ndo tumefahamu kuwa kumbe ni kweli walikua wana date,
Sasa vp kuhusu Kale ka ujauzito? Kaujauzito ambao inasemekana kwamba eti Kanumba alikua akimlazimisha Lulu atoe, na Lulu eti alikua akipinga kutoa mimba hiyo.

Hilo ndilo lingekua swali langu la kwanza kwa Actress Lulu Michael, mengine yangefata, Je wewe ungemuuliza nini?